Ili tuweze kupokea uponyaji wa kimsingi na tuishi maisha yenye afya, kila mmoja wetu lazima aelewe chanzo cha ugonjwa ni nini, na ni kwa jinsi gani tutapokea uponyaji. Kwa injili na kweli siku zote kuna pande mbili. Watu wasiokubali injili na kweli wamewekewa laana na adhabu, bali watu wanaokubali baraka na uzima vinawangojea. Ni mapenzi ya Mungu kwamba kweli ifichike kwa wale wanaojiona kuwa wenye hekima na akili, kama vile Mafarisayo na waalimu wa sheria. Pia ni mapenzi ya Mungu kwamba kweli ifunuliwe kwa wale ambao ni kama watoto, wanaoitamani na kufungua mioyo yao (Luka 10:21). Mungu ameahidi waziwazi baraka kwa wale wanaotii na kuishi kwa kufuata amri zake. Lakini pia amenakili kwa utondoti kuhusu laana na aina zote za magonjwa yatakayotupwa juu ya wale wasiotii amri zake (Kumbukumbu la Torati 28:1-68). Kwa kuwakumbusha Neno la Mungu watu wasioamini na hata baadhi ya waamini wanaolisahau, kazi hii inalenga kuwaweka watu kama hao katika njia ya sawa na kupata uhuru kutokana na magonjwa na maradhi.
Bitte wählen Sie Ihr Anliegen aus.
Rechnungen
Retourenschein anfordern
Bestellstatus
Storno







